Benin: Baraza la Seneti kumchagua rais wake wa kwanza
Wiki moja baada ya kuanzishwa kwake, Baraza la Seneti la Benin litamchagua rais wake leo Alhamisi, Agosti 6. Rais mpya wa Baraza la Seneti ambaye atachaguliwa kwa muhula wa miaka mitano, kama inavyoainishwa katika kanuni za ndani za taasisi hiyo, atachaguliwa kutoka miongoni mwa wanachama wa taasisi hiyo mpya. Ingawa uvumi umeenea, wengi wanashuku rais anayeondoka madarakani, Patrice Talon, kutaka kurudi kwenye uwanja wa siasa kupitia njia hii.
2026-08-06 05:04:40