Afrika Kusini: Jeshi lapelekwa katika vitongoji nyeti kupambana na magenge
Jeshi la Afrika Kusini limeanza kupeleka wanajeshi katika baadhi ya maeneo ya nchi ili kuwasaidia polisi katika mapambano dhidi ya uhalifu. Hatua hiyo imechukuliwa na rais Cyril Ramaphosa, na zaidi ya wanajeshi 2,000 wamehamasishwa. Hii si mara ya kwanza operesheni kama hiyo kufanyika, lakini wakati huu ni operesheni kubwa, inayolenga kukomesha shughuli za uchimbaji madini haramu na kurejesha utulivu katika vitongoji vinavyodhibitiwa na magenge.
2026-03-16 10:07:12