DRC: Watu kadhaa wafariki baada ya maporomoko ya ardhi ya Rubaya, mamia ya miili yafukiwa
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, siku tano baada ya maporomoko makubwa ya ardhi katika eneo la mgodi wa Rubaya katika jimbo la Kivu Kaskazini, idadi halisi ya vifo bado haijulikani. Kulingana na mamlaka za ndani, maporomoko ya ardhi yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 200. Hata hivyo, mashirika ya kiraia katika eneo la Masisi yanataja idadi ya vifo vya watu karibu 400.
2026-02-03 06:52:32