Rais wa Israel azuru Ethiopia, mshirika muhimu katika bara la Afrika
Rais wa Israel Isaac Herzog amewasili Ethiopia mnamo Februari 24 kwa ziara ya siku mbili. Katika ajenda kulikuwa na mikutano na mwenzake wa Ethiopia, Taye Atske-Selassie, pamoja na Waziri Mkuu Abiy Ahmed. Kwa Israel, ambayo uhusiano wake na washirika wake wa Afrika umezorota tangu Oktoba 7, Ethiopia inasalia kuwa mshirika muhimu katika bara hilo.
2026-02-25 08:36:26