Ushuru: Je, utawala wa Trump utafanya nini baada ya uamuzi wa Mahakama Kuu ya Marekani?
Mahakama Kuu ya Marekani imeamua siku ya Ijumaa kwamba sehemu kubwa ya ushuru uliowekwa na Donald Trump tangu kurudi kwake Ikulu ya Marekani ni kinyume cha sheria, na kuvunja nguzo muhimu ya ajenda yake ya kiuchumi. Hata hivyo, rais wa Marekani ametangaza jioni hiyo kwamba amesaini amri ya utendaji inayoweka ushuru mpya wa 10% duniani, kuanzia Februari 24, kwa kipindi cha siku 150.
2026-02-21 08:47:38