Mvutano waibuka tena kati ya Afrika Kusini na Israel, wanadiplomasia wawili wafukuzwa
Afrika Kusini imetangaza siku ya Ijumaa, Januari 30, 2026, afisa mmoja wa ubalozi wa Israel kuwa mtu asiyestahili. "Hatua hii inafuatia mfululizo wa ukiukwaji usiokubalika wa kanuni na desturi za kidiplomasia," imesema Idara ya Uhusiano wa Kimataifa. Kwa miezi kadhaa, maelezo rasmi ya ubalozi kwenye mtandao wa kijamii wa X yamekuwa maarufu kwa ukosoaji wake mkali dhidi ya serikali ya Afrika Kusini. Saa chache baadaye, Israel, nayo ilimfukuza mwanadiplomasia wa Afrika Kusini.
2026-01-31 07:44:28