Côte d'Ivoire: Afisa wa CNT wa Mali ahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kumtukana rais
Nchini Côte d'Ivoire, Mahakama ya mwanzo ya Abidjan imemhukumu Mahamadou Gassama kifungo cha miaka mitatu jela siku ya Ijumaa, Januari 30, 2026, kwa "kumtukana rais" na "kusambaza maneno ya machafu mtandaoni." Afisa huyu wa Mali kutoka Baraza la Kitaifa la Mpito (CNT) alikamatwa mnamo mwezi Julai 2025, kufuatia ziara ya kibinafsi nchini Côte d'Ivoire.
2026-01-31 07:57:17