Mashariki mwa DRC: Wakazi wa Uvira waomba mpaka na Burundi ufunguliwe tena
Wakazi na wafanyabiashara wa Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),wanaomba mpaka na Burundi ufuguliwe tena. Mwezi mmoja baada ya waasi wa AFC/M23 kuondoka katika mji wa Uvira, milio ya risasi imekoma, haisikike tena, lakini mpaka bado umefungwa. Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi anakumbusha kwamba hali ya usalama bado haijawa sawa ili mpaka wa nchi yake na DRC uweze kufuguliwa tena.
2026-02-19 11:23:07