පැටවීම

Slzii.com සෙවීම

සෙවීම (පුවත්)

Eti sijui kusoma? Wewe ndio ulikuwa unanililia ulipopokonywa Wizara ya Ulinzi, Jumwa ajibu Duale
ALIYEKUWA Waziri wa Utumishi wa Umma Aisha Jumwa wikendi alimjibu vikali Waziri wa Afya Aden Duale baada ya kutoa madai ya kutokuwa na uwezo wa kusoma na kuelewa stakabadhi za Baraza la Mawaziri walipokuwa serikalini. Bi Jumwa alimshutumu Bw Duale kwa unafiki na kusema matamshi yake yalilenga kumdhalilisha kisiasa. Alisisitiza kuwa alikuwa na uwezo kamili wa kuelewa shughuli za Baraza la Mawaziri. “Nilikaa nawe katika Baraza la Mawaziri na hakuna siku yoyote ulizungumza nami isipokuwa siku moja,” akasema Bi Jumwa. Alidai Bw Duale alimkasirikia baada ya kumpeleka mmoja wa magavana wa zamani kumwona Rais William Ruto. “Siku hiyo ulipozungumza nami ulikuwa na hasira kubwa, ukiniuliza kwa nini nilimpeleka gavana huyo kwa Ruto,” akasema. Bw Duale alikuwa amemshambulia Bi Jumwa Jumamosi jijini Mombasa, akidai wakati walipokuwa Barazani alikuwa akimsaidia kusoma na kuelewa baadhi ya stakabadhi za serikali. Alisema mara kadhaa Bi Jumwa alishindwa kueleza baadhi ya masuala yaliyokuwa kwenye hati hizo, hivyo akalazimika kumsaidia. Bw Duale alitoa matamshi hayo alipokuwa akikosoa uhusiano wa Jumwa na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua pamoja na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka. Hata hivyo, Bi Jumwa alimtaka Bw Duale kuacha kujaribu kuamulia Pwani upande wa kisiasa wa kuunga mkono. “Hutatuamulia Pwani mahali pa kupigia kura. Pwani ina viongozi wake na ikiwa unafikiri Pwani haina kiongozi, mimi niko hapa kwao,” alisema. Mbunge wa EALA Falhada Iman Dekow pia alilaani matamshi ya Bw Duale, akisema tofauti za kisiasa hazifai kugeuka kuwa vita vya kibinafsi dhidi ya viongozi wanawake. Alisema kila kiongozi ana haki ya kidemokrasia kuchagua upande wa kisiasa anaounga mkono.
2026-08-18 05:55:09

Kalonzo ataka Omollo ajiuzulu, adai ameshindwa kuzima uhuni
KIONGOZI wa Wiper, Kalonzo Musyoka amemtaka Katibu katika Wizara ya Usalama wa Ndani, Dkt Raymond Omollo kujiuzulu, akishutumu serikali kwa kushindwa kudhibiti uhuni wa kisiasa. Bw Musyoka pia alidai kuwa ukosefu wa usalama unaoshuhudiwa katika maeneo mbalimbali ni sehemu ya mpango wa kuunda mazingira yatakayotumiwa kuahirisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka ujao. “Wahuni wanaeneza hofu na hatuwezi kufuata mkondo huo. Katibu Omollo lazima ajiuzulu kwa sababu mkuu wake amekataa kumtimua ilhali kuna visa vya ukosefu wa usalama kila mahali,” akasema Bw Musyoka alipokuwa akizungumza katika Kanisa la Reedemed Gospel Kithimani, Kaunti ya Machakos. Alishangaa kwa nini vitendo vya kihuni vinaendelea licha ya Rais William Ruto kutoa hakikisho hapo awali kwamba serikali ilikuwa imemaliza tatizo hilo. Bw Musyoka alitaja ghasia zilizoshuhudiwa Homa Bay Jumapili, ambapo waandishi wawili wa habari walijeruhiwa na biashara kufungwa kuelekea mkutano wa Linda Mwananchi. Pia alirejelea vurugu zilizotokea katika eneobunge la Rongai Kaunti ya Nakuru Jumamosi, ambapo msafara wa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ulipigwa mawe na mikutano ya kisiasa kuvurugwa. Bw Musyoka pia alielekeza lawama zake kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), akisema Wakenya wanafuatilia kwa karibu kila hatua inayochukuliwa katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2027. “IEBC inapaswa kuwaruhusu Wakenya kuwachagua viongozi ambao hawajatwaliwa na serikali. Tulisema hatuwezi kuelekea katika uchaguzi ujao tukiwa na Smartmatic kama kampuni inayotoa programu ya uchaguzi, na tunajua michezo hii na lazima ikome,” alisema. Bw Musyoka aliandamana na Gavana wa Machakos Wavinya Ndeti, Mwenyekiti wa Wiper na aliyekuwa Mbunge wa Kigumo Jamleck Kamau, Seneta wa Machakos Agnes Kavindu na Naibu Gavana Francis Mwangangi. Bw Kamau alimuunga mkono Bw Musyoka katika azma yake ya kuwania urais 2027, akisema ana ushawishi wa kitaifa nje ya Ukambani. “Kalonzo si mwanasiasa wa Wakamba pekee, yeye ndiye rais wa sita wa Kenya. Kuanzia wikendi ijayo tutaanza ziara zetu za kisiasa na haki itakuwa msingi katika chama hiki,” alisema Bw Kamau. “Kalonzo ni mtu wa amani na 2007, kama hangeungana na Mwai Kibaki, nchi isingekuwa na amani. Amejitolea kwa dhati kwa Raila na sasa ni zamu yake. Hana doa. Ikiwa tunataka kiongozi mwenye amani, basi huyo ni Kalonzo Musyoka,” akaongeza Bw Kamau. Bw Musyoka pia alizungumzia utata wa bajeti katika Bunge la Kaunti ya Machakos, akiwataka MCA kuidhinisha bajeti hiyo ili serikali ya kaunti iweze kuendelea kutoa huduma kwa wananchi. “Bajeti si pesa za kibinafsi za gavana, kwa hivyo tushirikiane na tusonge mbele,” akasema kiongozi huyo wa Wiper. Gavana Ndeti alimtaka Rais Ruto na vyombo vya usalama kuchukua hatua madhubuti dhidi ya vitendo vya kihuni na kurejesha usalama nchini. Pia alimuunga mkono Bw Musyoka kuwania urais 2027, huku akiwakosoa madiwani kwa kuidhinisha nusu tu ya bajeti ya kaunti, ambayo alisema inaweza kugharamia mishahara pekee. “Bila bajeti hatuwezi kutoa huduma ambazo wananchi wetu wanahitaji. Nimewaita madiwani ili tukae pamoja kwa sababu ni sisi tutakaoipeleka kaunti hii mbele,” alisema Bi Ndeti.
2026-08-17 03:55:27

Thirty years on, a trial finally opens in Tupac Shakur's killing
Tupac Shakur seen here at Club USA, New York, March 30, 1994. Steve Eichner/Getty Images A former gang leader goes on trial Monday in Las Vegas over the decades-old murder of rapper Tupac Shakur, one of America's most high-profile unresolved murders. The proceedings, expected to last a month, will likely not make clear who fired the shots that killed the hip-hop legend on the night of September 7, 1996 while he was in Sin City to see a Mike Tyson boxing match. But prosecutors aim to show that the defendant, Duane "Keffe D" Davis, the onetime leader of the South Side Compton Crips, ordered the killing and provided the gun used to kill Shakur in a drive-by shooting. Davis, 63, faces life in prison without parole if convicted. The killing of Shakur, also known as 2Pac, is one of America's most celebrated cold cases, prompting endless debate among music fans over who did it and why. The rapper, who died at age 25, was a key figure in a hip-hop rivalry pitting the East Coast against the West Coast. Known for hits like "California Love" and "All Eyez on Me," Shakur -- the son of a Black Panther -- was raised in Harlem and Baltimore, but quickly became the epitome of a California bad boy when he signed with Los-Angeles based Death Row Records. The trial will revisit the battle between Death Row, founded by Marion "Suge" Knight, and Bad Boy Records, the East Coast label created by Sean "Diddy" Combs and starring Christopher "The Notorious B.I.G." Wallace (murdered in March 1997). Prosecutors say Death Row Records was protected by Mob Piru, a Los Angeles gang that was part of the wider Bloods alliance. Knight was affiliated with the group. Bad Boy Records had hired the rival group South Side Compton Crips, led by Davis, as bodyguards. After the Tyson fight at the MGM Grand casino, Knight and Shakur beat up Davis's nephew, Crips member Orlando "Baby Lane" Anderson, in retribution over an alleged assault of a Death Row employee. Davis was out for revenge, the prosecution says. Later that night, a white Cadillac carrying Davis, Anderson and others pulled up beside Shakur's car in Las Vegas. Shots were fired from the Cadillac, and Shakur was fatally wounded. - Compromising memoirs - The investigation sputtered for decades because of a lack of evidence, but the cold case was revived with the publication in 2019 of Davis's memoirs. In that book, Davis recounted that he was in the front seat of the Cadillac and that he handed a pistol to those in the back seat. But he does not say who opened fire on Shakur. Everyone else who was in the Cadillac that night has since died. These compromising revelations were consistent with remarks Davis had made previously to reporters. But this time, they came back to haunt him and he was arrested in September 2023. Davis has since backtracked and pleaded not guilty. "I'm innocent. I ain't killed nobody. Never did ever kill nobody," Davis said in March 2025 in an interview from prison with ABC News. "They don't have no evidence against me. They can't even put me in Las Vegas." Davis now says he was in Los Angeles the night of the Shakur killing and that he has never even read his own memoirs. He asserted that these were inflated by his co-author to generate book sales. "I just gave him details of my life," Davis said. "And he went and did his little investigation and wrote the book on his own." In the run-up to the trial, Davis's lawyers tried in vain to keep the book from being introduced as evidence, along with remarks he made in an interview with police in 2008 as a witness to the killing. The proceedings will open with jury selection, which is expected to take a week. Whatever the verdict is, it is unlikely to satisfy those close to Shakur. In May, the rapper's stepbrother Maurice Shakur filed a wrongful death lawsuit in civil court. "There remain individuals who were involved in Tupac's murder who, for 30 years, have not been held accountable for their crimes," his complaint says. The suit cites a recent TV documentary mini- series entitled "Sean Combs: The Reckoning," in which Davis says in an interview with police that Combs, now in prison himself, offered him $1 million to kill Shakur. ©Citizen Digital, Kenya
2026-08-10 09:48:10

South Sudan whistleblower abducted in Kenya released after two months
A South Sudanese whistleblower abducted in Kenya two months ago and transferred to his home country, where he was held at a military facility, has been released, his family said Monday. Athorbey Al-Gaddhaffy-Dit, 51, who also holds Kenyan citizenship, was living in Nairobi, where he had repeatedly warned that his life was in danger because he was exposing corruption linked to South Sudan's ruling elite, a representative told AFP in June. He was abducted at gunpoint by masked men as he left a casino in Nairobi two months ago, according to information his wife received from police. "We are very happy that Gaddhaffy has been returned to us after being abducted from Kenya and held in detention in Juba for almost two months," the family said in a statement. Al-Gaddhaffy-Dit was released on August 8 after investigations "did not reveal any wrongdoing", the family said. "We were never told why he was taken." The family said his health had deteriorated while in detention and that he was now receiving treatment in Kenya. Amnesty had earlier said that Al-Gaddhaffy-Dit was being held at a military facility and called on the Kenyan government to investigate. AFP has contacted the Kenyan foreign affairs ministry over the case but received no response. South Sudan is one of the world's poorest and most corrupt countries. A United Nations report last year detailed how government officials had stolen billions of dollars in oil money while leaving the population with hardly any essential services. Amnesty has previously warned that Kenya -- long considered a refuge for dissidents in a repressive east African region -- was increasingly complicit in allowing neighbouring countries to abduct their citizens. In November 2024, Ugandan opposition leader Kizza Besigye was kidnapped in Kenya and taken to a military court in Uganda, where he is facing treason charges. Turkish and Tanzanian dissidents have also been kidnapped on Kenyan soil. ©Citizen Digital, Kenya
2026-08-10 09:44:05

BATUK: Wabunge wadai Kenya haijaingia katika makubaliano na Uingereza
Wabunge wamesisitiza kuwa hakuna makubaliano mapya yaliyofikiwa kati ya Kenya na Uingereza kuhusu mkataba wa ushirikiano wa kijeshi na Kenya (BATUK). Kauli hiyo inajiri baada ya Uingereza kusema kuwa kumekuwa na maendeleo makubwa katika kutekeleza baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Bunge kuhusu Ulinzi. Uingereza ilisema maafisa wake wakuu walikutana na maafisa wa serikali ya Kenya, wabunge na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Masuala ya Kigeni Juni kujadili hatua iliyofikiwa. “Maafisa wakuu wa Uingereza walikutana na maafisa wa Serikali ya Kenya, wabunge na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Masuala ya Kigeni mwezi Juni kujadili maendeleo yaliyofikiwa hadi sasa,” ilisema taarifa hiyo. Uingereza pia ilisema taratibu za pamoja za kushughulikia mabomu na vilipuzi ambavyo havijalipuka zimekamilishwa. Miongoni mwa masuala mengine yaliyoshughulikiwa ni mahitaji ya ulinzi wa mazingira na matumizi ya ardhi, ambayo yamewasilishwa kwa mamlaka husika. Uingereza pia ilisema imeweka hatua mpya za kuzuia unyanyasaji wa kingono. Hata hivyo, Kamati ya Bunge kuhusu Ulinzi iliambia Bunge Jumanne kuwa mkataba huo bado haujaidhinishwa. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Nelson Koech, alisema makubaliano hayo hayawezi kuanza kutumika hadi masharti yaliyowekwa na Kenya yatimizwe. Bunge linataka vifungu vya 6(5) na 23 virekebishwe ili mauaji yawe chini ya mamlaka ya mahakama za Kenya. Wabunge pia wanataka BATUK iwe na mpango wa uwajibikaji kwa jamii unaohusisha maeneo inayofanyia shughuli zake. Bw Koech alisema kamati haitakubali mkataba unaokiuka Katiba au kudhalilisha Wakenya. Alisema kujumuishwa kwa mauaji katika vifungu vinavyopendekezwa kutaimarisha uwajibikaji na kuhakikisha wahalifu wa makosa hayo makubwa wanawajibishwa nchini. Mbunge wa Laikipia wa Kike Jane Kagiri aliunga mkono msimamo huo, akisema mtu yeyote anayefanya uhalifu nchini Kenya anapaswa kufikishwa mbele ya mahakama za Kenya. Kwa sasa, mkataba huo unaacha makosa kadhaa makubwa chini ya mamlaka ya Kenya, lakini mauaji hayajajumuishwa katika orodha hiyo. Hali hiyo imeibua wasiwasi kwamba Uingereza inaweza kudai mamlaka ya kushughulikia kesi za mauaji yanayohusisha wanajeshi wake. Bw Koech alisema masharti ya kamati bado hayajatimizwa licha ya serikali kutangaza kuanza tena kwa mafunzo ya pamoja ya kijeshi kati ya Kenya na Uingereza katika kituo cha BATUK, Laikipia. Alisema mazungumzo na kubadilishana mawasiliano kumeendelea, lakini Uingereza bado haijatoa ahadi ya kutosha kuhusu madai ya Kenya. BATUK imekuwa ikifanya shughuli nchini Kenya chini ya Mkataba wa Ushirikiano wa Ulinzi kati ya Kenya na Uingereza uliopitishwa mwaka 2016. Mkataba mpya uliwasilishwa Bungeni mwaka 2021 baada ya muda wa mkataba wa awali wa miaka mitano kuisha. Hata hivyo, Bunge la 12 lilimaliza muda wake kabla ya kuidhinisha mkataba huo. Mkataba huo uliwasilishwa tena kwa Bunge la 13 mwezi Novemba 2022. Baada ya kushirikisha wananchi, kamati ilipendekeza uidhinishwe kwa masharti kwamba vifungu vya 6(5) na 23 virekebishwe kabla ya kuanza kutumika.
2026-08-09 07:55:09

ඔයා කරන්නේ කුමක් ද?

0.022089958190918


පුවත්
පුවත්
කෙන්යාව
නවතම පුවත් සහ සිරස්තල
කෙන්යාව
පුවත්