Jeshi la Nigeria limetangaza Jumapili, Aprili 5, kwamba liliwaokoa waumini 31 waliotekwa nyara wakati wa sherehe za Pasaka katika kijiji cha Ariko, katika Jimbo la Kaduna, kaskazini magharibi mwa Nigeria. Watu watano waliuawa katika shambulio hilo, licha ya uwepo mkubwa wa vikosi vya usalama karibu na makanisa wakati wa sikukuu hiyo. Hata hivyo, wanakijiji na viongozi wa kidini wanapinga kauli ya jeshi.
2026-04-09 05:18:38