Nchini Burkina Faso, utawala wa kijeshi umetangaza Ijumaa jioni, Juni 26, 2026, kwamba unavunja mahusiano yake ya kidiplomasia na Ufaransa. Tangazo hilo lilitolewa kwenye televisheni ya taifa na msemaji wa serikali Pingdwendé Gilbert Ouédraogo. Burkina Faso ililaani, haswa, "harakati zisizoisha" za Ufaransa dhidi ya maslahi yake, kufuatia miaka kadhaa ya mvutano kati ya nchi hizo mbili. Ufaransa ilijibu, ikisema "inasikitishwa" na uamuzi wa "uhasama na usio na msingi."
2026-06-27 05:58:37