Nchini Sudan, wanamgambo wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) wametangaza mnamo Machi 24 kwamba wameuteka mji wa al-Kurmuk katika Jimbo la Blue Nile, kusini mashariki mwa nchi, kwenye mpaka na Ethiopia. Wanaungwa mkono na Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Sudan-Kaskazini (SPLP-N), kundi la waasi linaloongozwa na Abdelaziz el-Hilu.
2026-03-26 06:28:37