Nchini Kenya, mvua kubwa inaendelea kusababisha uharibifu mkubwa kote nchini. Watu themanini na mmoja wamepoteza maisha yao kutokana na mafuriko tangu mwanzoni mwa mwezi Machi, kulingana na takwimu za hivi karibuni za polisi zilizotolewa siku ya Jumapili, Machi 22. Zaidi ya familia 2,000 zimeyakimbia makazi yao.
2026-03-23 04:20:22