Nchini Mali, angalau watu wanane wameuawa na jeshi la Mali katika wilaya ya Yélimané ya mkoa wa Kayes, karibu na mipaka ya Mauritania na Senegal. Miili hiyo ilipatikana Machi 15 na 16, kufuatia kukamatwa kwa watu wengi na jeshi la Mali siku ya Ijumaa, Machi 13, katika vijiji kadhaa. Wakazi waliowasiliana na RFI wanaogopa kwamba ugunduzi huo mbaya hautaishia hapo.
2026-03-18 05:49:10