Waasi wa AFC/M23 wamedai kuhusika na shambulio la ndege zisizo na rubani kwenye Uwanja wa Ndege wa Bangoka katika jiji la Kisangani, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Siku ya Jumamosi, Januari 31, na Jumapili, Februari 1, mamlaka katika jimbo la Tshopo iliwashutumu waasi hao kwa kuhusika na mashambulizi yaliyolenga Uwanja wa Ndege wa Kisangani kabla ya jeshi na washirika wake kudhibiti hali.
2026-02-04 12:51:10