Sheria kuhusu mashirika yasiyo ya kiserikali imeanza kutumika siku ya Jumanne, Machi 3, nchini Angola, baada ya kupitishwa na Bunge linalodhibitiwa kwa kiasi kikubwa na chama tawala, MPLA. Sheria hii inaunda chombo cha utawala ambacho wanachama wake huteuliwa moja kwa moja na rais Joao Lourenço, waliopewa jukumu la "kufuatilia" shughuli na ufadhili wa mashirika yasiyo ya kiserikali.
2026-03-06 05:40:15