Waziri wa Mambo ya Nje wa Ghana, tangu siku ya Jumatatu, Agosti 17, amekuwa akizuru Urusi. Samuel Okudzeto Ablakwa alifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari na mwenzake wa Urusi, Sergey Lavrov. Wakizungumza na waandishi wa habari, wawili hao walijadili kuimarisha ushirikiano wao wa kidiplomasia na kiuchumi, pamoja na changamoto za usalama Afrika Magharibi na Sahel, na suala la raia wa Ghana kupigania jeshi la Urusi nchini Ukraine.
2026-08-19 11:06:29