Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa siku ya Jumanne, Juni 23, 2026, nchi saba za Ulaya zimetoa wito kwa wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) "kusitisha mara moja" shambulio lao dhidi ya mji wa El-Obeid, mji mkuu wa jimbo la Kordofan Kaskazini ambao uko chini ya udhibiti wa jeshi. Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ireland, Norway, na Uholanzi zinabaini kwamba "sasa kuna dalili za kuaminika za shambulio dhidi ya mji huo."
2026-06-24 05:45:02