Mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ambao unajumuisha nchi 16, ulimalizika Jumatatu jioni, Agosti 17, huko Durban, kwenye pwani ya mashariki ya Afrika Kusini. Kikao hicho cha faragha kiliendelea hadi jioni kabla ya Rais Cyril Ramaphosa kutoa hotuba yake ya kufunga. Na ilikuwa haiwezekani kwake kutozungumzia suala la uhamiaji, wakati nchi yake mnamo mwezi Juni ilikumbwa na maandamano dhidi ya wahamiaji wasio na vibali halali.
2026-08-18 05:58:34