Nchini Ethiopia, wakati mvutano huko Tigray ukiongezeka, serikali ya shirikisho inapoteza nguvu katika eneo la Amhara. Katika vita na serikali kwa miaka mitatu, waasi katika eneo la Amhara, pia wanajulikana kama Fano, wanapata tena nguvu na kudhibiti baadhi ya maeneo. Miji muhimu imetekwa tena, ikiwa ni pamoja na Debre Tabor, yapata kilomita 100 kutoka mji mkuu wa eneo hilo. Ndege zisizo na rubani zilishambulia mji huo mara kadhaa wiki iliyopita.
2026-02-16 06:44:21